TUIOMBEE BURUNDI
Nakumbuka katika mifano ambayo nilikuwa nikiitoa katika mitihani na hasa mitihani ya historia na uraia ilikuwa ni kuhusu namna gani nchi za afrika zinavyo mezwa na machafuko yanayosababishwa na siasa, vita  vya wenyewe kwa wenyewe, katika maandishi ya mwalimu wangu nakumbuka mpaka leo Jina la nchi ya afrika mashariki Burundi lilikuwa kati ya majina ya nchi yanayotajwa kuwa ni mifano ya nchi zenye vita, na machafuko ya kisiasa. Burundi ni  moja kati ya nchi masikini zaidi afrika na duniani kwa ujumla, watu wake wanaishi katika mazingira mabaya ya umasikini, machafuko ya vita yaliodumu kwa zaidi ya miaka 20 yameiharibu Burundi. Tokea mwaka 1993 mpaka 2006 watu wanauwawa na damu inamwangika tena damu inamwagika ya wasio na hatia wakiwawengi wanawake na watoto, mauaji ambayo yanachochewa na ukabila. Wa hutu na watutsi ambao wameshindwa kupendana na kuishi pamoja, chochoko zinaibukana na uvumilivu ukawashinda na kupigana jambo lilioichafua Burundi mpaka leo. Nchi hiyo ambayo imezungukwa na ardhi pande zote bila maji(nikimaanisha bahari na maziwa) inategemea vyanzo vya nchi jirani kuendelea mfano mzuri ni bandari ya Dar es salaam inayopakua mizigo mbalimbali inayosafirishwa kwenda Burundi . Leo hii takribani watu 400 wameuwawa kwa machafuko ya kisiasa yale yale kama yaliyotokea miaka iliyopita hata kabla sijajua, kuandika vyema, haya yote ni sababu ya rais Pierre Nkurunzinza kukataa achia wadhifa alioshikilia kwa mihula miwili.

Kutokuheshimu katiba ya nchi yake, na kutumia madaraka vibaya pierre nkurunzinza amefanya jambo ambalo watu wa nchi yake wanateseka hasahasa kina mama na watoto. Kiukweli hapakuwa na haja ya yeye kuendelea hodhi madaraka kwa muhula mwingine wa tatu, licha ya katiba inayo mwongoza kutokuwa na utaratibu wa namna hiyo. Kwa tafsiri ya haraka inaonyesha kuwa amesha sahau yalioikumba nchi anayoiongoza maana ni 2006 tu nchi ikaanza tulia. Nina jaribu tafakari ni aina gani ya washauri alionano maana nadhani hawakufanya kazi nzuri, nina uhakika walikuwepo na kwa mazingira ya nafasi aliyonanyo ni watu werevu na wenye ustadi wa kunyambua na wanaoaminika walikuwa sambamba nae. Iweje leo raia takribani 200,000 watafute hifadhi nchi ya jirani Tanzania, licha ya kuwa nchi mama yao ina ardhi ya kuwalea lakini kwa ukatili wa mtu mmoja leo hii hawana tena amani, ile historia ya nyuma imerudi na kuitafuna nchi yao, na kuwabatiza majina mapya, ‘’ WAKIMBIZI’’.

Nina andika ukurasa huu nikiwa na masikitiko sana, nina waza maneno ya Tony Blair aliyoyatoa mwaka 2001 kuwa afika ni kovu katika dhamiri yetu, akasisitiza ya kuwa dunia kama jumuiya  inatakiwa kuiangalia afrika na kuiponyesha maana isipofanya hivyo, afrika itakuwa imezama katika maovu na kuwa na hasira. Haya maneno yananifanya kuona namna gani nchi za magharibi zinavyoiona afrika, zinaona afrika kama janga, gonjwa hatari la kuambukiza ambalo linatakiwa kutibiwa mapema, maana uvunjifu wa katiba kufaidisha waliojuu, unaonekana kwa dhahiri bila woga ndani ya nchi za kiafrika na unasababisha maafa makubwa kama yanayotokea leo Burundi. Kila kukicha milio ya risasi, na miili kuonekana ovyo mitaani ikiwa na matundu ya risasi kichwani. Hii ina maanisha nini kuna kikundi cha watu kinafanya haya kinalenga watu, kwa uelewa wangu wa mambo ya kijasusi, kupigwa risasi ya kichwa ni ishara ya kuua kwa uhakika bila kuwa na mashaka ya mpigwaji kupona. Na hii inaonesha ya kuwa mauaji haya yanalenga watu. Jaribio la kupinduliwa Nkurunzinza liliposhindwa liliashiria kuwa kuna viongozi wa juu wa kijeshi hawamuungi mkono rais na ni wasaliti nadhani hilo lilimkasirisha sana Nkurunzinza na kufanya uapisho mapema bila kutangazwa hata uchaguzi kuwa wa mashaka mashaka.

Jumuiya za afrika, hasahasa afrika mashariki zinatakiwa kuangalia suala hili kwa umakini kubwa sana maana idadi kubwa ya wakimbizi inazinyemelea nchi jirani na Burundi na Tanzania ambazo ziko karibu, mzigo mkubwa unazielemea kuwahudimia wakimbizi hao, licha ha hilo afrika imefika wakati ipumizike na majanga ya kuletwa na sisi, miaka iliyoipita imetosha kwa vifo vya watu kwa maelfu, sasa ni wakati wa kujipanga na kuleta maendeleo, kwa haya yanayotokea Burundi ni ishara ya kurudia makosa makubwa ambayo yanamaumivu makali sana.

Naisihi jumuiya ya Umoja wa Afrika kuiokoa Burundi na vita, kuokoa maisha ya watu yanayozidi potea kila kukicha, kuvamiwa kwa kituo cha kijeshi kuanashiria kuwa kuwa kikundi cha watu wasio na hofu na dhamira yao ni kuangamiza, polisi na jeshi hawawezi tuliza machafuko kwa nguvu zao sio kwa namna ambavyo jamii inawachukulia hasahasa waandamanaji. Hebu waafrika werevu waweke akili zao pamoja na kuikoa Burundi, ifike siku tuyaache haya katika vitabu vya historia tusivyo taka  vifunua kwa kizazi kilichopita. 

Mungu Ibariki Afrika. Mungu Iokoe Burundi.


Comments