TUENDELEE
Ninakumbuka kipindi
niko shuleni, hasa katika wakati wa michezo pale wanafunzi wenzangu na mimi
tulipokuwa tukiweka miili yetu sawa kiafya kwa kukimbia na kucheza mpira.
Lakini jambo ninalo likumbuka sana ni wakati ule ambapo,niliujua mchezo wa mbio
za kupeana vijiti .Mantiki yake ina
umaridadi mkubwa katika dhana ya umoja hasa pale washindani mnapokuwa ‘’fiti’’.
Kwa hali ya sasa, wakati huu, dakika hii ninapoandika makala hii Februari 13
mwaka 2016, ni miezi miwili tu imepita tangu tufanye uchaguzi na kuaga mwaka
2015. Yaliojiri mwaka jana yamebaki mwaka jana sasa ni kuendelea na kazi, na kwa vile dhamira ya kiongozi wa
juu wa nchi yetu ni ‘’ Kazi Tu!’’ basi
kijiti changu kimepewa mimi mwingine mwenye mwili wa nyama uleule lakini mwenye
nia, ari na morali zaidi.
Tangia nifahamu juu ya
tarehe mosi ya kila Januari, na usiku wa kuieleta kwake nimekuwa nikiwaza sana
kauli mbalimbali za watu wanaonizunguka juu ya upeo wao, pale wanaposema ‘ ‘
huu ni mwaka mpya ’’. kwa akili ya kawaida kwa binadamu mwenye kuweka dhana
kama hii katika hali ya asili katika tafsiri ya haraka haraka ni kama hivi;
mwaka mpya ni kitu ambacho kila muda muafaka ukifika vitu vinavyo akisi umaana
wake vinabadilika na kuwa upya, miezi siku majira, na tarehe. Huu mtazamo upo
ndani ya watoto wengi, na ulikuwa ndani yangu wakati nilipokuwa bado mtoto, na
katika hali ambayo kwa kweli si ya kawaida kwa hali niliyo nayo sasa kila
kulipokuwa kukikucha na kuikaribisha asubuhi ya tarehe Mosi, kwangu ilikuwa ni
siku tofauti licha ya kwamba hali ya hewa, mazingira, watu na nafsi yangu vyote
vilikuwa vilevile. Na kikubwa nilichokuja gundua ni kwamba si kuuona Mwendelezo,
upya ulitawala.
Dunia inaendelea na
mambo yake, IS bado wanatawala sehemu mbalimbali Syria na Libya wakisambaza
hofu kwa watu, nchi za ulaya bado zinapokea wakimbizi toka Syria, Africa
Magharibi,Libya Na yemen, wanaowapokea bado wanajadiliana ni njia ipi watumie
kuwakwepa, wajerumani bado wanaendelea kujitahidi wastiri japo kuwa wajerumani
wenzao pia hawawataki kabisa wageni. Licha ya kuwa tarehe zinabadilika na
kutuletea miaka, mambo yetu hayabadiliki, mwaka
mpya una ashiria kuwa ; muda wako ulipewa katika kipindi husika
umekwisha, muda zaidi umewadia , Je? Tasmini yako ya mambo uliyoyafanya kwa
mwaka mzima ina mashiko sanjari na hilo ,endelea na mambo yako kwa muda huu wa nyongeza uliopewa na asili.
Kwa upeo wangu nafikiri mwaka mpya uliitwa ‘’Mwaka Mpya ’’ kwa sababu ; mwongozo
wa muda, siku na majira unao tafsiriwa
na kalenda ya mwaka husika umefikia kikomo na kalenda mpya inawadia, na dhahiri
ina maanisha kuwa mwaka umekwisha, na
mfumo mpya(kalenda) wa siku kwa wanadamu umewadia. Kuwa dhahiri kidogo kwa sasa
Tanzania na Dunia kwa ujumla ina utumia mfumo wa kalenda ya Gregory iliyoanza
kutumika mnamo mwaka 1582.
Kwa wanadamu kila siku
inakuja na mambo mapya na fursa mbalimbali za kutumia, kwa werevu wanazitumia
vilivyo kama vile hawataiona kesho, na wakifanikiwa kuiona kesho na kwa bahati
nzuri kesho hiyo ikaangukia Tarehe Mosi
ya Mwaka Mpya, nina uhakika hawata kuwa na budi kuendelea na jitihada
zao za kujipatia Riziki. Mwalimu na mwanafunzi mwaka mpya unawapa wote Jua,
Mwanga Wa mwezi, Usiku na Mchana namna wanavyotumia nafasi hizo ni juu yao,
jambo la msingi ni kuacha dhana ya kuweka mambo mapya mbele kila mwaka mpya
unapofika wakati ya kale bado hayaja maliziwa na wakati mwingine hata kufanyiwa
kazi. Kuendelea pale ulipoacha ni jambo linaloonyesha kuwa unajali, na
umehamasika na kile unacho kifanya cha msingi ni kujitahidi kumaliza kwa heri
na fanaka. Maana kila mwaka unakuja na mambo yake. Ukweli ni kwamba mwaka mpya
unafaida kwa watu walio katika mrengowa kushoto kwa namna moja au nyingine,
maana nimeshuhudia watu wakiweka nadhiri kuacha mambo maovu, dhambi, na kuwa
wapya na kujisafisha nafsi zao yote hayo ni kuhakikisha Mwaka mpya unapokelewa
kwa heri na watu safi, wanaondelea kuishi lakini wakiishi kwa mrengo na fikra
mpya.
Tuendelee na jitihada
za kuifanya nchi yetu Tanzania kuwa nchi yenye amani na umoja, utawala wa sheria
uimarike, haki na uhuru wa kila raia kuheshimiwa, na chini ya uongozi wa Dk.
John Magufuli nchi yetu ing’are katika sekta nyeti; Elimu,afya na uchumi. Licha
ya kuwa Rais wetu kaapishwa mwaka jana, juhudi na kazi zake zinaendelea, mwaka
mpya umempa nafasi ya kuona hali ya nchi na kupata muda wa ziada kuendelea
itengeneza nchi na kwa ushirikiano wetu watanzania tutafika tunapopataka,
tusome vitabu, kwa maarifa na kufikiri zaidi. Tuendelee.
Comments
Post a Comment