Sikutaka kabisa kuangalia wakaniambia" fumbua macho
taswira yake sio ya kama kichwani kwako", wakanishawishi na kuwahadaa
pigeni kwa wingi picha mnato, pilipili haiwashi daima, itilie ndani ya mchuzi wa
sato utamu wa leo si wa kesho .
Batili imekuwa baraka, nyaraka za siri ziko nje kama
talaka, sina stara tena tunu zangu ndo wanazozitaka, hawaoni haja ya kukinga
maji ya mvua, kazi yao ni kusubiri maji ya bomba kila mwaka.
Tumieni walau akili kidogo tangu lini kichwa kilicho
unda meli ya kubeba mizigo, watu hata punda, kiseme" hata sarafu yaweza
elea kama Titanic , huenda itavuka mabara kama mkiomba," ninaona bora
kurudi zama za kale kutumia maji na jiwe kujiremba, karne hii vioo vya jamii
vyanitenda kama solemba.
Siku hizi hakuna tena haya, kukuonesha akiba ya
mwenzangu ruksa, uvumilivu haupo na kuacha maembe mabichi yaive ni nadra
sasa. Nasikia hatupandi tena miti ya
vivuli kwavile embe huwa tamu unaposhushia na umbea wa insta.
Chujio halito baki kutimiza azma ya mpishi, maana nayo
yaona katika talakilishi yamenikifu bila ubishi, utu wetu jalala: karatasi,
vyupa, na maganda ya ndizi tutupiwe sisi. Si mnapenda kuitwa mabingwa wakati
hamtii amri, kufanyika gaga si kupona donda, fanyeni utaratibu wa kumpa salome
achambue hizo karanga, mkumbusheni tunu zake asiziweke rehani na protini muhimu
kwa afya kuilinda.
Rafiki bakuli na chupa ya maji vyote hukata kiu, lakini
kipindupindu kitakuhusu vimelea wakihusika unaisikia mbiu.
Comments
Post a Comment