Takwimu
za sensa, zinaonyesha zaidi ya asilimia 50 ya jumla ya watu waishio Tanzania ni
wanawake. Toka kuanzishwa kwake, mwaka 1961 wanawake wa Tanzania,w amekuwa na mchango
mkubwa katika uchumi, siasa na elimu, hil halina shaka.
Vivyo hivyo, katika
anga za kimataifa, Utalii umekuwa ukitupa nafasi kubwa ya kujitanua na
kujitangaza, hasa kwa vivutio vyetu ikiwemo Serengeti-yenye Zaidi ya KM za mraba
30,000, moja katika ya maajabu saba ya dunia, papo hapo imetupa heshima kushinda
tuzo ya hifadhi bora barani Afrika(2019). Kina-mama na utajiri wa asili vyote
ni tunu zetu, abadani hakuna wa kubeza thamani yao, lakini kwanini tuna
vishusha thamani kiasi hiki kwa kusukuma agenda zisizo na msingi?
Siku
kadhaa nyuma, kumekuwa na mirindimo ya kashfa, kubeza, kusimanga kwa watu: walio
ona habari za Serengeti na ushindi wake kuwa njema machoni/masikio pao kushinda
habari chafu za “Teleza” na vitendo vyao, kuitwa na makundi ya watu mbalimbali
kuwa ni watu wasio ona huruma kwa kina-mama huko mkoani Kigoma, wanaopitia gathabu
ya wanaume wabakaji wanaoitwa “Teleza”. Sababu ya kwanini wanaitwa jina hilo
sihitaji kusema, inasikitisha kueneza habari zao za laana, ila kwa umuhimu wa Makala
hii ni tija kueleza na kulaani matendo yao.
Tabia
zao zenye kuleta hofu mioyoni mwa watu wote: wanaume na wanawake, zimeanza
rindima toka mwaka 2016, ambapo vyombo vyetu
vya habari vilitupa undani wake, ambapo wamejeruhi wanawake, kwa kuwacharanga
mapanga pale walipo jaribu kupambana, kulinda utu wao, Kituo Cha Sheria na Haki
za Binadamu (LHRC) kime repoti kwa kina juu ya matukio haya na kulaani vitendo
hivi visivyo vya kiungwana na vinavyo ogofya jamii zetu.
Mwaka,
huu kesi kadhaa zimeibuka mkoani Kigoma, zinazo husisha vitendo hivyo hivyo, LHRC
imeonyesha takribani matukio zaidi ya 40 ambayo yametukia ndani ya mkoa kwa
mwaka huu. Jeshi la polisi kama ilivyo ada, limejikita kuhakikisha watu hawa
wanakamatwa na kutiwa nguvuni, kuweka usalama na utulivu kwa wananchi.
Vyombo
vya habari vimetumia nafasi yake ya kuwapa-wananchi-taarifa yakinifu juu ya
matukio haya. Ni jukumu la waandishi wa habari kufuata miiko na kanuni za
uandishi bora kuhakikisha mizani ya usambazaji habari imefuata vyema. Lakini,
utata umeibuka pale Rais wa Tanzania, Dr. John Joseph Pombe Magufuli, alipo toa
duku duku lake, narudia duku duku lake juu ya vyombo vya habari kuto ipa habari
ya Ushindi wa Hifadhi ya Serengeti nafasi moja kwa siku moja katika vichwa
vikuu vya habari, katika magazeti yake.
Nipende,
kuwa fahamisha (kwa wale ambao hawajapata pitia hili) yakuwa katika uandishi wa
habari yeyote kuna vitu muhimu kwa kufuata ikiwemo, umihimu, ukaribu-wa-habari-
na-wasomaji, muda na matokeo ya habari yenyewe. Kama, mwandishi wa habari
kijana, niliona habari ya Serengeti kukidhi vigezo KABISA bila shaka yeyote, vivyo
hivyo habari ya kinara wa ubakaji “Teleza” huko Kigoma, inakidhi vigezo vyote,pia.
Cha
kushangaza, maneno ya Rais yamegeuzwa na kuweka katika mizani isiyo sawa, na
wengine kuingia katika mtego wa kujenga hoja uitwao kwa lugha ya kigeni “
Strawman Fallacy” , mtego huo unaonesha namna watu wanavyo weza tumia hoja yako
kinyume na matakwa/nia ya maneno yako na kupindisha uhalisia wa mambo katika
hoja wanazo taka ziwe.
Katika
Mitandao ya kijamii hasa Twitter, kurasa yangu, ilisheheni, maoni ya watu
waliokuwa wakisema ya kwamba, ushindi wa Serengeti hauna mashiko kwa wananchi
wa kawaida maana , hawaendi katika mbuga hizo, wengine wakidiriki kusema hakuna
utu sasa pale tunapo shadidia tuzo na si kutetea wanawake wahanga.
Yote
hayo juu, ni mlundikano wa hisia tupu na si hoja. Nipende kusema ya kwamba,
maneno ya kiongozi wa taifa yalichukuliwa katika muktadha na maana tofauti
kabisa, nina amini ya kwamba hakuwa na nia ya kudharau wala kukebehi vitendo
vya hao mafedhuli wasio na haya kwa wanawake, ila nina amini, kama mtanzania,
alitamani kuona Tanzania, walau kwa masaa 24 ikisomeka vyema katika vichwa vikubwa
vya habari kwenye magazeti kupitia tunu yake Hodari SERENGETI, na habari ya
mhalifu huyo kupewa pia nafasi yake lakini katika vichwa vidogo, na si
kutokuchapishwa kabisa.
Hoja
ilikuwa tuchague, kuendeleza anika aibu ya nchi yetu ama, kwa namna moja au
nyingine ipa “SHAVU” Tanzania katika duru za kimataifa na kuzidi ongeza watalii
Zaidi na fedha za kigeni, kutanua sekta ya utalii itakayo leta ajira Zaidi na
fursa zingine za kibiashara.
Ilikuwa
ni kuchagua, kuendelea kuzungumzia maumivu (ambayo ni lazima kwa wananchi
kujulishwa) katika vichwa vya habari ama kuitangazia dunia juu ya utajiri
tulionao, maana ilikuwa ni nafasi moja tu na haitojirudia tena KAMWE.
Kama
ilivyo ada uwezo wa kunyambua na kuya angalia mambo kwa jicho pevu umeonekana
wazi katika hili, kuwa dhaifu. Ni muhimu kuangazia tasfiri na kuyachambua
maneno katika muktadha husika na kuhakikisha hoja zinazo jengwa zinawekwa
katika mizani imara yenye kushibisha azma ya kuanika madhaifu na kuinua mema.
Hebu
basi japo mara moja kwa mwaka, tumpe MAMA TANZANIA heshima yake ya kimataifa
pale anapo tupa baraka zake, ni hilo tu.


Comments
Post a Comment